You are here > News > Saturday News

Last Updated: 21.8.2010
ENGLISH | SWAHILI | SPORTS
Uingereza kuendelea kuwa mshirika wa Tanzania -Balozi
UINGEREZA imesema itaendelea kuwa mshirika wa Tanzania katika maendeleo kwa kuwa mazingira yake kisiasa yanavutia uwekezaji.Balozi wa Uingereza nchini, Diane Corner alisema hayo jana jijini Dar es Salaam.Alisema ikilinganishwa na nchi nyingine za Afrika Mashariki, Tanzania ni tulivu, ina rasilimali za kutosha na inavutia kwa uwekezaji.
"Tanzania ni nchi tulivu na mazingira yake yanavutia uwekezaji. Uingereza imeamua kuiweka (Tanzania) katika ramani yake ya uwekezaji," alisema Balozi Corner na kubainisha kuwa mwaka jana, Waingereza 55,000 walitembelea Tanzania kwa ziara za kitalii.
Alisema mbali na utalii huo, takriban Waingereza 7,000 wanaishi nchini kwa shughuli mbalimbali.
Balozi Corner alisifia vyombo vya habari nchini, akisema vimenatoa mchango mkubwa katika kukuza demokrasia.
"Nisingependa kuzungumzia chombo kimoja bali mtazamo wangu kuhusu vyombo vya habari. Kwa kweli vimechangia sana hali hii ya kuwa na demokrasia ya kuridhisha," alisema.
Alisema vyombo vya habari vya Tanzania vimekuwa huru kuliko ilivyokuwa miaka ya tisini na kwamba, sasa watu wanapata habari zaidi.
Awali mkurugenzi wa Mwananchi Communications, Sam Shollei alieleza kuwa anaamini mabadiliko katika siasa za Tanzania, yanaweza kutokea katika chaguzi zijazo kutokana na mabadiliko mbalimbali.
"Nimeanza kuona wimbi la vijana likijiingiza kwenye siasa na wazee wakianguka. Hii inaashiria kuwa kutakuwa na mabadiliko makubwa baada ya Rais Kikwete," alisema Shollei.
Kabla ya kukutana na Shollei na baadaye wahariri wa magazeti yanayochapishwa kampuni hiyo, Balozi Corner alitembelea vitengo mbalimbali, ikiwemo kiwanda cha uchapishaji, ambako alivutiwa na mtambo wa kisasa wa kuchapisha magazeti unaomilikiwa na MCL
Rushwa ilikithiri kura za maoni CCM-Makweta
WAZIRI wa zamani wa serikali ya awamu ya kwanza Jackson Makweta, ambaye ameangushwa kwenye kura za maoni za CCM, amevunja ukimya akisema utaratibu uliotumika kupata wagombea wa CCM ulikithiri kwa rushwa.
Makweta, ambaye amekuwa mbunge wa Jimbo la Njombe Kaskazini mkoani Iringa tangu mwaka 1995, pia alisema wengi wa wanachama wa CCM waliopiga kura hawakuwa na uelewa wa kutosha kujua umuhimu wa kura na kwamba wingi huo ulisababisha Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kushindwa kufanya kazi ipasavyo.
Makweta, ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Elimu na Utamaduni, alisema hayo juzi katika kipindi maalumu cha mjadala kuhusu mchakato wa kura za maoni ndani ya CCM kilichorushwa na Idhaa ya Kiswahili ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC).
Mjadala huo ulimjumuhisha Profesa Paramagamba Kabudi, John Lusinde, ambaye ni mgombea ubunge wa jimbo la Mtera kwa tiketi ya CCM, na naibu katibu mkuu wa chama tawala nchini Uganda(NRM), Maiki Mukula.
Make Comments About this Article click here