You are here > News > Thursday News

Last Updated: 9.9.2010
ENGLISH | SWAHILI | SPORTS
Mpakistan akamatwa kwa kuchana noti ya Sh 5,000
POLISI mkoani Mwanza limemtia mbaroni raia wa Pakistan baada ya kuchana hadharani noti mmoja ya Sh 5,000.
Tukio hilo, lilitokea jana saa 11:45 asubuhi wakati Mpakistani huyo ambaye jina lake tumelihifadhi akiwa miongoni mwa abiria ambao walikuwa uwanja wa ndege Mwanza wakikaguliwa kwa ajili ya kuingia kwenye ndege ili kunza safari ya kutoka Mwanza hadi Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari jana Kamanda wa polisi mkoani Mwanza, Simon Sirro alisema Raia huyo wa Pakistani alitenda kosa hilo hadharani huku akishuhudiwa na abiria wenzake ambao pia walikuwa wakisubiria kusafiri kwa ndege hiyo ya shirika la Precision.
Kamanda Sirro alisema raia huyo wa Pakistani ni mfanyakazi katika shirika la Catholic Refugees Service (CRS) linalojishughulisha na kutoa huduma na misaada kwa wakimbizi.
“Akiwa kama abiria wengine wakati wakiwa katika ukaguzi kwa ajili ya kuingia ndani ya ndege, huyu alitoa noti moja ya Sh 5,000 na kuanza kuichana chana vipande, kwa kitendo hicho abiria waliokuwepo walikasirishwa na kitendo hicho na kutoa taarifa kwa maofisa usalama ambao walikuja na kumkamata,” alieleza.
Alisema baada ya kuzungumza naye kwa kina alionekana kutokuwa na sababu za msingi na hivyo kuamua kumchukulia hatua na walimkabidhi kwa ofisa wa polisi na kufikisha katika kituo ambako waliendelea kumshikilia kwa mahojiano zaidi.
“Tunavyo vipande vya noti ambayo alivichana kama ushahidi, kitendo hiki kinaonyesha dharau kubwa kwa fedha yetu na taifa letu, na kinaonyesha kukosa ukosefu wa heshima.” alifafanua zaidi Kamanda Sirro.
Makamba: CCM haing'oi mabango ya mgombea urais
WAKATI Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa akitaka CCM kuacha kutumia mabango ya mgombea urais wa chama hicho yenye picha za Ikulu, chenyewe kimetunisha misuli kikisema hakitaondoa mabango yake kwani hakuna picha za taasisi hiyo nyeti ya nchi.
Mvutano huo umekuja siku moja baada ya Baraza la Vyama vya Siasa, kutaka CCM iache kutumia nyenzo za Ikulu yakiwemo mabango ambayo picha zake zimeandaliwa kwa gharama za Ikulu.
Hata hivyo, akizungumza na gazeti hili jijini Dar es Salaam jana, Makamba alifafanua mambo matatu ya msingi kuhusu mabango ya mgombea urais wa chama hicho Jakaya Kikwete.
Make Comments About this Article click here